• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Kongwa District Council
Kongwa District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kongwa

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala
      • Mipango, Takwimu & Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Idara ya Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Idara ya Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Maliasili
      • Idara ya Maendeleo ya Jamii
      • Ujenzi & Zima moto
      • Mazingira na Usafi
    • Vitengo
      • Kitengo cha Sheria
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Manunuzi
      • Kitengo cha Uchaguzi
      • Kitengo cha Ufugaji Nyuki
  • Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Ardhi
    • Madini
    • Biashara
    • Viwanda
    • Mawasiliano
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Huduma za Ardhi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za TEHAMA
    • Usimamizi & Ufuatiliaji wa Miradi
    • Huduma za Ushauri na Ufundi
    • Ruzuku ya Kunusuru Kaya Masikini
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba ya Vikao
  • Miradi
    • Miradi Inayoendela
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Kilimo
      • Utawala
      • Maendeleo ya Jamii
      • Nishati
    • Miradi iliyokamilika
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Kilimo
      • Utawala
      • Maendeleo ya Jamii
      • Nishati
  • Machapisho
    • Sheria ndogo ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
    • Mpango Mkakati wa Halmashauri
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
    • Majarida
    • Gazeti la Serikali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • Video za Shughuli za Maendeleo
  • Michezo
    • Michezo
    • Sanaa

TASAF yaipongeza Halmashauri ya Wilaya ya Kongwa

Imewekwa: March 14th, 2025

Mwenyekiti wa kamati ya mpango wa kunusuru kaya masikini Tanzania (TASAF) Taifa Bwana Peter Ilomo ameupongeza uongozi wa Halmashauri ya Wilaya ya Kongwa kwa juhudi za usimamizi mzuri wa miradi ya nyumba mbili za walimu katika shule ya Sekondari Chitego.

Bw. Ilomo ameyasema hayo katika ziara yake Wilayani Kongwa alipotembelea na kujionea mradi wa nyumba mbili za walimu zilizopo katika Kata ya Chitego Kijiji cha Chitego wilayani Kongwa ambapo amewaomba walimu pamoja na uongozi wa Kijiji kuhakikisha nyumba hizo zinatunzwa ili ziweze kuleta matarajio yaliyokusudiwa.


Aidha Bw Ilomo ameonyesha kufurahishwa na shuhuda za wanufaika wa (TASAF) hususani wanaume kutumia ruzuku walizopewa kwaajili ya kuinua uchumi wa familia na jamii zao na kubainisha kuwa kuna baadhi yao hutumia vibaya fedha hizo kwa malengo yasiyokusudiwa na mfuko na kuomba wanufaika watumie vizuri ruzuku.

Nae Mkurugenzi Mtendaji wa TASAF Taifa kutoka idara ya ajira za muda, Mhandisi Tadei Shirima ameelezea kuwa wananchi waliopata fursa ya kupata miundombinu kama iliyojengwa Chitego ni wachache kwani ndani ya Halmashauri ya Wilaya Kongwa ni Kijiji kimoja cha Chitego hivyo anaamini kutokana na uhitaji wao watazitunza vizuri nyumba hizo.

Kwa upande wake Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Kongwa Bw. Fortunatus Mabula amemshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuwatazama watanzania na kuendelea kusimamia wananchi kupata huduma muhimu, jambo linalowezesha TASAF kuwafikia wananchi na kubadili maisha yao kiuchumi. Vilevile Kaimu Mkurugenzi emeeleza Imani yake kuwa walinzi wa kwanza wa miradi ya nyumba hizo watakuwa walengwa wenyewe hivyo nyumba hizo zimekabidhiwa kwa watu sahihi watakaotunza miundo mbinu hiyo.

Nae mratibu wa TASAF mkoa wa Dodoma Bi. Josephine Pascal amewataka walengwa kutambua fedha zinazotolewa na TASAF ni za Serikali ya awamu ya sita na ni juhudi za Mhe. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan, fedha ambazo zinatolewa kwaajili ya kuwakwamua wananchi dhidi ya umasikini.

Vilevile Diwani wa Kata ya Chitego Mhe. Peter Kalunju ameomba uongozi wa TASAF kujenga mabweni katika shule ya Chitego ili kuwasaidia wanafunzi wanaotembea umbali mrefu kufika shuleni kwa uharaka ili kupata muda wa kutosha wa kujisomea katika mazingira ya shule.

Pamoja na hayo wakitoa shuhuda zao walengwa wa TASAF wilayani Kongwa wamesema kuwa fedha wanazopata zimewasaidia kuinua uchumi wa familia zao kwa kufanya mambo mbalimbali kama kujenga nyumba za bati, kusomesha watoto, kununua mifugo, kununua mashamba na chakula na kutoa shukrani zao za dhati kwa uongozi mzima wa TASAF Pamoja na Serikali ya awamu ya Sita.

Matangazo

  • Majina ya mipaka ya vijiji na vitongoji vilivyopo katika eneo la Halmashauri ya Wilaya ya Kongwa. October 16, 2024
  • TANGAZO LA MAELEKEZO YA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA 2024. October 16, 2024
  • Tangazo la nafasi za ajira za mkataba October 07, 2024
  • Tangazo la kufunguliwa kwa dirisha la utoaji mikopo kwa vikundi vya wanawake, vijana na watu wenye ulemavu- Oktoba 1 2024 October 02, 2024
  • Tazama Yote

Habari Mpya

  • MGOGORO WA MPAKA CHIGWINGWILI - HOGORO KUTAFUTIWA UFUMBUZI.

    May 08, 2025
  • VIKUNDI VYASISITIZWA KUWA NA USHIRIKIANO MZURI NA VIONGOZI PAMOJA NA WATAALAM

    May 05, 2025
  • VIKUNDI 21 VYAKABIDHIWA MIKOPO YA ASILIMIA KUMI YA HALMASHAURI

    April 28, 2025
  • DC MAYEKA AKABIDHI MISAADA

    April 27, 2025
  • Tazama Yote

Video

zoezi la uandikishwaji daftari la Mpiga Kura kuanza 11-20 Oktoba, 2024
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu Mbalmbali
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Miongozo
  • Miradi iliyokamilika
  • Miradi inayoendelea
  • Taarifa kwa Umma
  • Zabuni
  • Kituo cha Biashara (OSBC) Kongwa
  • Orodha ya Madiwani na Mawasiliano

Viunganishi Linganifu

  • Time huru ya Uchaguzi
  • Tovuti ya Taifa
  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti ya Ajira
  • Wakala ya Serikali Mtandao (e-GA)

Watembeleaji wa Dunia

world map hits counter

Rekodi ya Watembeleaji

Counter Widgets

Ramani

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkurugenzi Mtendaji Wilaya

    Anuani ya Posta: S.L.P 57 Kongwa, Dodoma

    Simu ya Mezani: +255 26 2370031

    Simu ya Mkononi: +255 713399349

    Barua pepe : ded@kongwadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti
    • Tahadhari kwenye Barua pepe

Copyright ©2022 Kongwa District Council . All rights reserved.