• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Kongwa District Council
Kongwa District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kongwa

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala
      • Mipango, Takwimu & Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Idara ya Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Idara ya Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Maliasili
      • Idara ya Maendeleo ya Jamii
      • Ujenzi & Zima moto
      • Mazingira na Usafi
    • Vitengo
      • Kitengo cha Sheria
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Manunuzi
      • Kitengo cha Uchaguzi
      • Kitengo cha Ufugaji Nyuki
  • Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Ardhi
    • Madini
    • Biashara
    • Viwanda
    • Mawasiliano
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Huduma za Ardhi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za TEHAMA
    • Usimamizi & Ufuatiliaji wa Miradi
    • Huduma za Ushauri na Ufundi
    • Ruzuku ya Kunusuru Kaya Masikini
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba ya Vikao
  • Miradi
    • Miradi Inayoendela
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Kilimo
      • Utawala
      • Maendeleo ya Jamii
      • Nishati
    • Miradi iliyokamilika
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Kilimo
      • Utawala
      • Maendeleo ya Jamii
      • Nishati
  • Machapisho
    • Sheria ndogo ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
    • Mpango Mkakati wa Halmashauri
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
    • Majarida
    • Gazeti la Serikali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • Video za Shughuli za Maendeleo
  • Michezo
    • Michezo
    • Sanaa

Katibu talawa wa mkoa wa Dodoma ashiriki chakula cha mchana pamoja na wanafunzi wa darasa la saba

Imewekwa: September 3rd, 2024



Na. Mbonea E. Masha


Katibu tawala mkoa wa Dodoma mhe. Kaspar K. Mmuya leo tarehe 3 Septemba, 2024, amehudhuria hafla fupi ya kukutana na wazazi pamoja na wanafunzi wa darasa la saba katika shule ya msingi Msingisa Kata ya Sagara Wilaya ya Kongwa ili kuungana nao katika chakula cha mchana pamoja na kuwatakia heri katika mitihani ya kuhitimu elimu ya msingi itakayofanyika hivi karibuni.

Bwana Kasper Mmuya ameambatana na Afisa taaluma mkoa wa Dodoma, mwalimu Justin Machela,  Afisa elimu msingi wilaya ya Kongwa Mwl. Magreth Temu na Afisa tarafa ambapo kila mmoja alipata nafasi ya kuwapongeza wanafunzi wa darasa la saba kwa hatua waliyofikia na kuwaasa waendelee kusoma kwa bidii ili wafanye vizuri mitihani yao na waweze kutimiza ndoto zao.

Akisoma risala mbele ya mgeni rasmi kwa niaba ya jumuiya ya shule ya msingi Msingisa, mwalimu mkuu alianza kwa kurejea kauli mbiu ya shule isemayo, “Hamu kubwa ya kushinda, hushinda hofu ya kushindwa, tunastawi tulikopandwa.” kugusia ujasiri waliojengewa wanafunzi kukabili changamoto zilizo mbele yao. Akiendela kusoma risala mwalimu mkuu akaongeza kuwa jamii ya shule ya Msingisa ina imani kubwa sana kuwa mwaka 2024 utakuwa ni mwaka wa maajabu kwakuwa wanatarajia kufanya vizuri zaidi katika matokeo ya mitihani ya darasa la  nne na la saba na kufanya shule kuwa na wastani mkubwa

Aidha mwalimu mkuu akagusia changamoto ambazo zimekuwa zikirudisha nyuma maendeleo ya shule ikiwemo baadhi ya wazazi kuwashawishi wanafunzi wao kufanya vibaya katika mitihani ya taifa ya darasa la saba na kupelekea idadi kubwa ya wanafunzi kufeli, changamoto nyingine ni baadhi ya wazazi wachache kukataa kuchanga michango ya lishe shuleni ambayo ingewafanya wanafunzi wapate chakula wakiwa shule.

Mwalimu mkuu wa shule ya Msingisa, ametoa shukrani zake za dhati na kumshukuru Mhe Kaspar kwa kutembelea shule hiyo na kuonyesha imani yake kuwa ugeni wa katibu tawala wa mkoa wa Dodoma katika shule hiyo, utafanyika kuwa baraka na kufanya mwaka 2024 kuwa mwaka wa mafanikio makubwa katika jamii ya shule ya msingi ya Msingisa. Mwalimu mkuu katika risala yake, ametoa shukrani zake za dhati kwa Afisa elimu wa Wilaya mwalimu Magreth Temu ambaye amekuwa akitembelea shule ya Msingisa mara kwa mara na kuwaasa na kuwashauri kwenye mambo mengi yenye manufaa kwa shule hiyo. Mwalimu mkuu hakusita kumshukuru mkurugenzi mtendaji wa Halmashauri ya Kongwa Dr. Omary Nkullo kwa kuwapatia bati ambazo zimetumika katika ujenzi wa nyumba ya kisasa ambayo itatumika kama nyumba ya mwalimu itakapokamilika.

Akijibu risala, mgeni rasmi Mhe. Kaspar Mmuya alianza kwa kushukuru jumuiya yote ya shule ya msingi Msingisa kwa kuandaa hafla hiyo na kuhudhuria kwa wingi. Katiba hotuba yake, Bwana Kaspar ametumia msemo wa elimu ni ufunguo wa maisha kusisitiza umuhimu wa elimu katika kusaidia kuona fursa na kuzitumia fursa zikaleta maendeleo. Mgeni rasmi amegusia swala la wazazi kukataa kuchangia lishe shule na kuwaeleza kuwa mtoto asipokula shule inaathiri uwezo wake wa kuwa makini katika masomo na amekemea swala la wazazi kuwashawishi watoto wao wafanye vibaya kwenye mitihani yao ili wasifaulu kwenda sekondari kwani kufanya hivyo ni kutomuwezesha mtoto asome na kupata maarifa ya kutafsiri changamoto za maisha akiwa peke yake sababu watoto hao hawatakuwa na wazazi milele na kuwashawishi kufanya vibaya ni kutengeneza kizazi cha watu tegemezi ambao wengi wao watajiingiza kwenye shughuli haramu zenye kuvunja sheria ili kujipatia mahitaji yao ikiwemo wizi, unyang’anyi na mengineyo na kuleta hasara kwa jamii na taifa kwa ujumla.

Aidha Mhe. Kaspar Mmuya amesisitiza kuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt Samia Suluhu Hassan anafanya kazi kubwa kuhakikisha mtoto anapata elimu na ndio maana anajenga madarasa hivyo wazazi wanapaswa wamuunge mkono mheshimiwa rais kuhakikisha juhudi zake zinazaa matunda na hazikwamishwi katika ngazi ya familia. Mhe. Kaspar amemaliza hotuba yake kwa kuwatakia kila la heri wanafunzi wote wa shule ya msingi Msingisi na kusema kuwa hana shaka kuwa wanafunzi wote waliojiandikisha watafaulu mitihani yao na kuendelea na masomo yao ili kutimiza ndoto zao.

Mtihani wa taifa wa kuhitimu darasa la saba utafanyika kuanzia Jumatano ya tarehe 11 Septemba mpaka tarahe 12 Septemba 2024 ambapo shule ya msingi Msingisi ina wanafunzi 118 waliojiandikisha na wanaotarajia kufanya mtihani huo.

pichani ni Katibu tawala Mkoa wa Dodoma pamoja na Afisa elimu msingi Wilaya ya Kongwa Mwl. Magreth Temu wakipata chakula pamoja na wanafunzi na wazazi.

Matangazo

  • Majina ya mipaka ya vijiji na vitongoji vilivyopo katika eneo la Halmashauri ya Wilaya ya Kongwa. October 16, 2024
  • TANGAZO LA MAELEKEZO YA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA 2024. October 16, 2024
  • Tangazo la nafasi za ajira za mkataba October 07, 2024
  • Tangazo la kufunguliwa kwa dirisha la utoaji mikopo kwa vikundi vya wanawake, vijana na watu wenye ulemavu- Oktoba 1 2024 October 02, 2024
  • Tazama Yote

Habari Mpya

  • MGOGORO WA MPAKA CHIGWINGWILI - HOGORO KUTAFUTIWA UFUMBUZI.

    May 08, 2025
  • VIKUNDI VYASISITIZWA KUWA NA USHIRIKIANO MZURI NA VIONGOZI PAMOJA NA WATAALAM

    May 05, 2025
  • VIKUNDI 21 VYAKABIDHIWA MIKOPO YA ASILIMIA KUMI YA HALMASHAURI

    April 28, 2025
  • DC MAYEKA AKABIDHI MISAADA

    April 27, 2025
  • Tazama Yote

Video

zoezi la uandikishwaji daftari la Mpiga Kura kuanza 11-20 Oktoba, 2024
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu Mbalmbali
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Miongozo
  • Miradi iliyokamilika
  • Miradi inayoendelea
  • Taarifa kwa Umma
  • Zabuni
  • Kituo cha Biashara (OSBC) Kongwa
  • Orodha ya Madiwani na Mawasiliano

Viunganishi Linganifu

  • Time huru ya Uchaguzi
  • Tovuti ya Taifa
  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti ya Ajira
  • Wakala ya Serikali Mtandao (e-GA)

Watembeleaji wa Dunia

world map hits counter

Rekodi ya Watembeleaji

Counter Widgets

Ramani

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkurugenzi Mtendaji Wilaya

    Anuani ya Posta: S.L.P 57 Kongwa, Dodoma

    Simu ya Mezani: +255 26 2370031

    Simu ya Mkononi: +255 713399349

    Barua pepe : ded@kongwadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti
    • Tahadhari kwenye Barua pepe

Copyright ©2022 Kongwa District Council . All rights reserved.