• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Kongwa District Council
Kongwa District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kongwa

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala
      • Mipango, Takwimu & Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Idara ya Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Idara ya Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Maliasili
      • Idara ya Maendeleo ya Jamii
      • Ujenzi & Zima moto
      • Mazingira na Usafi
    • Vitengo
      • Kitengo cha Sheria
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Manunuzi
      • Kitengo cha Uchaguzi
      • Kitengo cha Ufugaji Nyuki
  • Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Ardhi
    • Madini
    • Biashara
    • Viwanda
    • Mawasiliano
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Huduma za Ardhi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za TEHAMA
    • Usimamizi & Ufuatiliaji wa Miradi
    • Huduma za Ushauri na Ufundi
    • Ruzuku ya Kunusuru Kaya Masikini
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba ya Vikao
  • Miradi
    • Miradi Inayoendela
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Kilimo
      • Utawala
      • Maendeleo ya Jamii
      • Nishati
    • Miradi iliyokamilika
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Kilimo
      • Utawala
      • Maendeleo ya Jamii
      • Nishati
  • Machapisho
    • Sheria ndogo ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
    • Mpango Mkakati wa Halmashauri
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
    • Majarida
    • Gazeti la Serikali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • Video za Shughuli za Maendeleo
  • Michezo
    • Michezo
    • Sanaa

AMANI IWE MJADALA BILA KUJALI ITIKADI.

Imewekwa: December 9th, 2024

Mkuu wa Wilaya ya Kongwa Mhe Mayeka Simon Mayeka amewataka wananchi wote wa Kongwa kuimarisha amani iliyopo bila kujali itikadi za siasa, dini na ukabila.

Mhe Mayeka ameyasema hayo katika sherehe za kilele cha maadhimisho ya siku ya Uhuru wa Tanzania Bara yaliyofanyika katika ukumbi wa chuo Cha veta Kongwa na kuhudhuriwa na viongozi mbalimbali wa dini na Serikali na makundi ya wananchi mbalimbali ambapo amesisitiza kuwa amani iliyopo katika nchi ya Tanzania haikutokea tu ila ni kazi ya watangulizi wetu.

"kama tutaacha umoja upendo na amani, maendeleo hayana maana yoyote, miaka 63 ya uhuru tumepata maendeleo makubwa inatupasa tutengeneze mazingira mazuri ya kufikia maendeleo zaidi" amesema Mhe. Mayeka.

Kwa upande wake Mkuu wa Wilaya ya Kongwa Mstaafu Mhe. Ole Saitabahu ameeleza kuwa Taifa la Tanzania limepiga hatua kubwa sana ya maendeleo na lazima kila mwananchi ajipongeze kwa hatua iliyofikiwa

Ndugu. Saitabahu ameweka wazi kuwa enzi za uongozi wake alitembea kwa miguu wakati akitekeleza majukumu yake sababu hakukuwa na gari la ofisi na pia ameweka wazi kuwa shule nyingi hazikuwa na ubora, akibainisha kuwa hata vyoo havikuwepo ukilinganisha na miaka hii ambapo miundombinu ya kila sekta imeboreshwa na viongozi wote wa Serikali Wana vyombo vya usafiri kurahisisha utendaji kazi wao.

Nae katibu wa CCM Wilaya ya Kongwa Bi Joyce Mkaugala amefafanua kuwa mada ya Uhuru wa Tanzania Bara inapoongelewa huwa inaambatana na kumbukumbu ya Chama Cha TANU kilichoanzishwa kwaajili ya kupigania uhuru kipindi cha hayati baba wa Taifa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere.

Akiongea kwa niaba ya kikundi cha wanawake na Samia Bi. Debora Chambo amesema kuwa miaka 63 ya Uhuru wa Tanzania Bara, nchi ya Tanzania imepiga hatua katika upande wa kupigania haki za wanawake na kupambana na masuala ya ukatili wa kijinsia na watoto.

Sherehe za kilele cha maadhimisho ya siku ya Uhuru wa Tanzania bara zimebeba kauli mbiu ya, “UONGOZI MADHUBUTI NA USHIRIKISHWAJI WA WANANCHI NI MSINGI WA MAENDELEO YETU.” Kwa dhumuni la kusambaza falsafa ya wananchi kushirikishwa katika hatua za maamuzi ili kuleta maendeleo ya Taifa kwa ujumla.

Matangazo

  • Majina ya mipaka ya vijiji na vitongoji vilivyopo katika eneo la Halmashauri ya Wilaya ya Kongwa. October 16, 2024
  • TANGAZO LA MAELEKEZO YA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA 2024. October 16, 2024
  • Tangazo la nafasi za ajira za mkataba October 07, 2024
  • Tangazo la kufunguliwa kwa dirisha la utoaji mikopo kwa vikundi vya wanawake, vijana na watu wenye ulemavu- Oktoba 1 2024 October 02, 2024
  • Tazama Yote

Habari Mpya

  • MGOGORO WA MPAKA CHIGWINGWILI - HOGORO KUTAFUTIWA UFUMBUZI.

    May 08, 2025
  • VIKUNDI VYASISITIZWA KUWA NA USHIRIKIANO MZURI NA VIONGOZI PAMOJA NA WATAALAM

    May 05, 2025
  • VIKUNDI 21 VYAKABIDHIWA MIKOPO YA ASILIMIA KUMI YA HALMASHAURI

    April 28, 2025
  • DC MAYEKA AKABIDHI MISAADA

    April 27, 2025
  • Tazama Yote

Video

zoezi la uandikishwaji daftari la Mpiga Kura kuanza 11-20 Oktoba, 2024
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu Mbalmbali
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Miongozo
  • Miradi iliyokamilika
  • Miradi inayoendelea
  • Taarifa kwa Umma
  • Zabuni
  • Kituo cha Biashara (OSBC) Kongwa
  • Orodha ya Madiwani na Mawasiliano

Viunganishi Linganifu

  • Time huru ya Uchaguzi
  • Tovuti ya Taifa
  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti ya Ajira
  • Wakala ya Serikali Mtandao (e-GA)

Watembeleaji wa Dunia

world map hits counter

Rekodi ya Watembeleaji

Counter Widgets

Ramani

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkurugenzi Mtendaji Wilaya

    Anuani ya Posta: S.L.P 57 Kongwa, Dodoma

    Simu ya Mezani: +255 26 2370031

    Simu ya Mkononi: +255 713399349

    Barua pepe : ded@kongwadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti
    • Tahadhari kwenye Barua pepe

Copyright ©2022 Kongwa District Council . All rights reserved.